Mahali: @ Kituo cha Mabasi Stesheni - Ilala
Ada ya Tukio: @ 50,400 /= per Child
Tarehe: 2018-03-24 - 2018-03-29
Muda: 8.00 Hours - 16.00 Hours
NHIF inautangazia umma kuwa itaendesha zoezi la usajili wa bima ya afya kwa watoto wa chini ya miaka 18 - TOTO AFYA KADI, katika eneo la kituo cha mabasi cha Stesheni-Ilala, kuanzia Tar 24-03-2018 hadi Tar 29-03-2018 saa 2 asubuhi hadi saa 10 jioni kila siku.
Uje na mchango wa Tsh. 50,400, nakala ya cheti cha mtoto cha kuzaliwa (tangazo la uzazi endapo mtoto ana chini ya miezi 6 na hana cheti) na picha ndogo (passport size) ya mtoto. Kwa maelezo zaidi wasiliana nasi kupitia simu na. 0800110063 bila malipo.
Huduma bora za matibabu ni haki yako na ni dhamana yetu.
